

Mkamaria
Marcus Rashford ameaga rasmi Barcelona baada ya klabu hiyo kuamua kutomsajili kwa mkataba wa kudumu. Mshambuliaji huyo wa England pia hatarudi kwa mkopo mwingine, hivyo safari yake ya kucheza Camp Nou imefikia mwisho.
Kupitia ujumbe wa hisia, Rashford aliwashukuru viongozi wa klabu, wachezaji wenzake na mashabiki kwa kumpa kipindi ambacho hatakisahau maishani.
"Nina shukrani za dhati kwa kila mmoja ndani ya klabu kwa kufanya muda wangu hapa kuwa wa kipekee na usiosahaulika."
Aliendelea kusema:
"Nimefurahia kila dakika niliyokuwa hapa na nitabeba kumbukumbu hizi maalum milele. Naiombea klabu na mashabiki wote mafanikio makubwa msimu huu. Visca Barça."
Baada ya kuhitimisha safari yake Barcelona, Rashford sasa anarejea Manchester United kuanza maandalizi ya msimu mpya, huku mustakabali wake ukiendelea kuwa moja ya gumzo kubwa katika dirisha la usajili.

